UZINDUZI WA JOHN LISU AKIZINDUA ALBAM YAKE YA PILI "UKO HAPA"YENYE NYIMBO KUMI NA NANE(18), KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUMBILEE HALL JIJINI DAR ES SALAM.
Uzinduzi huo umefanyika leo,na mgeni Rasmi ni Mheshimiwa Stephani Wasira pamoja na wachungaji kutoka sehemu mbalimbali na waimbaji waliomsindikiza akiwepo Rose mhando,Christina shusho,Christina kilahiro,Abwene mwasongwe, Solomon mkubwa, Glory celebration pamoja na wengine wengi.

Waziri wa Nchi,ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu),STEPHA WASIRA akionyesha albam ya" Uko hapa"John Lisu yenye nyimbo (18), na kushoto ni mchungaji Mwakibolo wa kanisa la Mito ya baraka lilopo J angwani na kulia ni Mkurugezi wa kampuni la Msama promosion,Alex Msama ambaye ni mdhamin wa uzinduzi huu.
JOHN LISU AKIPIGA GITA HUKU AKIIMBA.
Huyu ndiye muimbaji wetu wa nyimbo za Injili sifa na kuabudu John Lisu aliyejazwa Roho mtakatifu ambaye amefanikiwa kutoa albam mbili ya kwanza iki itwa "Jehova yu hai"yenye nyimbo kumi (14),na ya pili ni "Uko Hapa" zenye nyimbo kumi(18).
Hawa ni waimbaji wa John Lisu wakiwajibika jukwaani kwenye uzinduzi wa albam ya "Uko hapa".
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni